Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2018
Picha
KILICHOPO NYUMA YA PESA ZA VIJANA NA WANAWAKE HALMASHAURI  Kwenye kila halmashauri nchini Tanzania kuna pesa zimetengwa kwa ajili ya maendeleo ya vijana na wanawake. Pesa hizo zimetengwa kwa ajili ya kuwapa vikundi vya kimaendeleo ambavyo vimeundwa na hao vijana pamoja na hao wanawake. Na ili kila kikundi kiweze kupata hizo pesa ni lazima kiwe na shughuli maalumu ya uzalishaji mali ambazo zinawaingiza kipato sambamba na hivyo vikundi kutambulika kisheria yaani visajiliwe katika ofisi zenye mamlaka husika ambazo zipo chini ya usimamizi wa afisa maendeleo.   KWANINI VIJANA NA WANAWAKE? Kwa sababu haya makundi mawili ndio chachu ya maendeleo katika jamii na taifa kwa ujumla kwa kuwa vijana ni taifa la kesho hivyo hakuna budi kuwawezesha sasa ili kesho waweze kusimama wenyewe na ukimuwezesha mwanamke mmoja ni sawa umeiwezesha jamii nzima kwa kuwa wanawake wanaangaliwa kama chachu ya mabadiliko na maendeleo katika jamii na taifa kwa ujumla kulingana na walivyobarikiwa. ...
Picha
    DHANA YA VIKUNDI VYA MAENDELEO NA ASASI ZA KIBENKI Katika jamii kuna vikundi vya maendeleo na vikundi hivi vya maendeleo kazi yake kubwa ni kuhakikisha kuwa vinatengeneza fursa mbalimbali kwa wanachama na jamii kwa ujumla kupitia huduma au bidhaa zao. MAANA YA VIKUNDI VYA MAENDELEO Vikundi vya maendeleo ni vikundi vyote vinavyojihusisha na shughuli mbalimbali za uzalishaji mali katika jamii yaani vikundi hivi vinakuwa na kazi zao maalumu wanazozifanya ambazo zinawaingiza kipato na kuwasaidia katika jitihada zao za kupambana na umaskini.mfano wa shughuli zinazofanywa na hivi vikundi vya maendeleo ni ukulima wa mazao,ufundi seremala na ufundi washi,utengenezaji wa sabuni na bidhaa mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya binadamu na shughuli nyingine nyingi sana. IDADI YA WATU Kumbuka hivi ni vikundi kwa ajili ya kutengeneza faida ili wanachama wake waweze kujikwamua na changamoto mbalimbali katika maisha yao sambamba na umaskini.hivyo wataalamu wa maendeleo ya jami...